Baluchistan
Mandhari

Baluchistan, Balochistan au Baluchestan[1] (بلوچستان) ni eneo linalokaliwa na Wabaluchi. Imegawiwa kati ya Pakistan, Irani na Afghanistan.
Hapa kuna vitengo vifuatavyo:
- Jimbo la Balochistan katika Pakistan (km² 347.190 , wakazi milioni 12.3, nusu yao Wabaluchi)
- Mkoa wa Sistan na Baluchistan katika Irani (km² 181,785, wakazi milioni 2.5, zaidi ya nusu Wabaluchi)
- Katika Afghanistan eneo la Wabaluchi limegawiwa kati ya wilaya za Nimruz, Helmand na Kandahar, idadi yao ni takriban 600,000.
Idadi ya Wabaluchi inakadiriwa kuwa milioni 10. Wengine huishi nje ya Baluchistan hasa katika miji mikubwa ya nchi zao. Kuna pia Wabaluchi katika Afrika ya Mashariki na mababu zao walichukuliwa kama askari na Sultani wa Zanzibar wakati wa karne ya 19.
Marejeo
[hariri | hariri chanzo]- ↑ Tofauti za tahajia ya jina inatokana na namna tofauti za kutamka jina hili ambalo linaadikwa na wenyeji kwa herufi za Kiarabu ambako hakuna tofauti baina ya u/o na e/i.
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Baluchistan kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |